Shilingi kwa ya pili; mbona hazishabihiani?
Ninaomba maafisa wa Benki Kuu au Hazina Kuu ya kitaifa wajibike na kutueleza sisi Wakenya kinagaubaga, ni sarafu ipi ya shilingi yetu ndio halisi? Ni bayana kwamba sarafu ni kigezo muhimu cha dhamani ya mali. Hivyo basi, kigezo hicho inafaa kiwe ama kifanywe dhabiti. Ni mara ngapi maafisa kutoka idara ya vipimo na ubora huwashambulia wenye maduka wanaotumia ratili ambazo hazina usawa na ulinganifu wa wastani uliyowekwa? Si mawe ya ratili zote yamepewa uzito sawia ili kuhakikisha kwamba viwango vinatoshelezwa? Itafaa zaidi kama tutatumia sarafu moja ya kutegemewa na wala tusipewe shiligi moja ya fedha iliyo kubwa, ingine ya fedha iliyo ndogo na hata isitoshe moja ya shaba iliyo ndogo kushinda hata senti kumi! Na tuambiwe kuwa shilingi ni shilingi bora tu iwe na mhuri wa Benki Kuu Ni ukweli noti zetu zinatosheleza ubora wa ulinganifu wa kimuondo ila, duniani kote inajulikana kuwa ni pesa za sarafu ndizo zenye kuamika zaidi kwa maana zinawakilisha dhamani y