Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia 2013

FALSAFA

Falsafa ni nini? Falsafa ni juhudi ya kuuliza, kufahamu na kujibu maswali sugu kwa tafakuri. FALSAFA YA KIAFRIKA NA YA ULAYA FALSAFA YA KIAFRIKA Inaweza kugawanywa katika sehemu zifuatazo mbili. Yani, falsafa ya Kiafrika ni aidha Kiujumla: Falsafa yoyote ile ambayo itaguzia maudhui ya kiafrika au itatumia mbinu za kiafrika kukidhi madhumuni yake. Kimaalum: Falsafa ile tu imetokana na mtu ambaye ni Mwafrika au an uzao wa Kiafrika. Falsafa ya Kiafrika inachukua daraja tatu 1. Uhenga-tamaduni: Weledi wa mambo yote ya mila ya watu wa jamii fulani. Hapa kuna Falsafa-tamaduni: Weledi wa mila na desturi za jamii na unamilikiwa na watu wote wa jamii hiyo ila, wazee ni wahenga zaidi kuliko watoto. Falfasa-uhenga: Weledi wa mambo ya mila na tamaduni za jamii zilizomo kwenye mhenga mmoja mashauri. Falsafa-shehe: Mweledi wa mambo ya mila na tamaduni za jamii pamoja na mambo mengi ya malimwengu 2. Falsafa-itikadi: Uanzilishi ama uzinduzi wa mfumo wa fikira wa ku

IKTISADI

Iktisadi ni nini? Iktisadi ni sayansi ya kijamii inayo husika na jinsi matarajio na mahitaji mengi ya jamii yanawezatoshelezwa na raslimali haba. Wanaiktisadi ni wanasayansi na kwa hivyo wanawezakutoa kauli mbili: kauli thabiti na kauli ya kimapendekezo. Kauli thabiti: Hizi ni kauli zinazowezadhibitishwa kwa kufanyiwa utafiti, kwa mfano: bei zikishuka, bidhaa zitanunuliwa kwa wingi zaidi. Kauli pendekezi: Haya ni mapendekezo tu, kwa mfano: Serikali inafaa ipunguze ushuru kwa bidhaa muhimu. Hivyo basi, wanaiktisadi mara nyingi hawaakifikiani. KUUNDA MODELI/NATHARIA 1. Jumlisha dhana 2. Tunga miongozo 3. Dhibitisha miongozo 4. Matokeo yakitoshana na = ukweli wa mambo 5. Basi inakuwa natharia Modeli husaidia kurahisisha kuelezea dhana tofauti tofauti. Katika somo la kiuchumi, modeli/natharia huchukua mfano ya chati. Raslimali za kiuchumi: Pia zinawezaitwa Viungo vya Kuzalisha Uchumi navyo ni 1. Ardhi – Raslimali yote halisi iliyopo paha

Shilingi kwa ya pili; mbona hazishabihiani?

Picha
Ninaomba maafisa   wa Benki Kuu au Hazina Kuu   ya kitaifa wajibike na kutueleza sisi Wakenya kinagaubaga, ni sarafu ipi ya shilingi yetu ndio halisi? Ni bayana kwamba sarafu ni kigezo muhimu cha dhamani   ya mali. Hivyo basi, kigezo hicho inafaa kiwe   ama kifanywe dhabiti. Ni mara ngapi maafisa kutoka idara ya vipimo na ubora huwashambulia wenye maduka wanaotumia ratili   ambazo hazina usawa na ulinganifu wa wastani uliyowekwa? Si mawe ya ratili zote yamepewa uzito sawia ili kuhakikisha kwamba viwango vinatoshelezwa?  Itafaa zaidi kama tutatumia sarafu moja ya kutegemewa na wala tusipewe shiligi moja ya fedha iliyo kubwa, ingine ya fedha iliyo ndogo na hata isitoshe moja ya shaba iliyo ndogo kushinda hata senti kumi! Na tuambiwe kuwa shilingi ni shilingi   bora tu iwe na mhuri wa Benki Kuu  Ni ukweli noti zetu zinatosheleza ubora wa ulinganifu wa kimuondo ila, duniani kote inajulikana kuwa ni pesa za sarafu ndizo zenye kuamika zaidi kwa maana zinawakilisha dhamani y