Shilingi kwa ya pili; mbona hazishabihiani?




Ninaomba maafisa  wa Benki Kuu au Hazina Kuu  ya kitaifa wajibike na kutueleza sisi Wakenya kinagaubaga, ni sarafu ipi ya shilingi yetu ndio halisi?

Ni bayana kwamba sarafu ni kigezo muhimu cha dhamani  ya mali. Hivyo basi, kigezo hicho inafaa kiwe  ama kifanywe dhabiti. Ni mara ngapi maafisa kutoka idara ya vipimo na ubora huwashambulia wenye maduka wanaotumia ratili  ambazo hazina usawa na ulinganifu wa wastani uliyowekwa? Si mawe ya ratili zote yamepewa uzito sawia ili kuhakikisha kwamba viwango vinatoshelezwa? 

Itafaa zaidi kama tutatumia sarafu moja ya kutegemewa na wala tusipewe shiligi moja ya fedha iliyo kubwa, ingine ya fedha iliyo ndogo na hata isitoshe moja ya shaba iliyo ndogo kushinda hata senti kumi! Na tuambiwe kuwa shilingi ni shilingi  bora tu iwe na mhuri wa Benki Kuu 

Ni ukweli noti zetu zinatosheleza ubora wa ulinganifu wa kimuondo ila, duniani kote inajulikana kuwa ni pesa za sarafu ndizo zenye kuamika zaidi kwa maana zinawakilisha dhamani ya madini yaliomo na sio tu mhuri wa benki.  Basi ni heri wataalamu husika waanze kulinganisha sarufi za pesa zetu ili tuwe na moja tu ambayo ni wastani  kutuelekeza kutathmini  bei halisi ya bidhaa zilizoko sokoni, gharama ya maisha na dhamani ya pesa za kigeni.

 Edwin Musonye

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FALSAFA

IKTISADI

Katiba kwenye mtazamo wa miraba tatu (Sehemu II-I): Kugeuza katiba bila Kura ya maoni