Jinsi mawaziri wa fedha walivyodhibiti viwango vya riba na akiba
Kiwango cha riba na akiba za mabenki ni chombo muhimu sana kwa kukuza biashara na uchumi. Hii ni kwa sababu viwango viliopo huchangia kuvutia ama kutimua wateja ambao mara nyingi huwa ni wafanyibiashara. Kiwango cha kukopa kikiwa juu, wakopi hushindwa kulipa madeni yao. Lakini, wakopeshaji wakiwa na mioyo ya kibepari kama Shailoki wa Venisi, hukimbilia kuuza mali yao bila huruma wakidai walipwe kwa ‘haki na haka ya hati yao’. Kenya, kama nchi, imelaumiwa kwa kuwa na kiasi kidogo cha uwekezaji wa akiba. Hata hivyo, wakosoaji wamekataa kutambua kuwa faida ya mtu kuziacha pesa benki ni duni. Hii ni kufuatia kuwa mvuvumko wa bei ya bidhaa mara nyingi huwa juu kushinda mapato yanaolipwa na hazina za benki au taasisi zingine za kifedha. Hali hii huwatoa watu hamu ya kuwaacha pesa kwa akaunti ya hazina. Lakini juhudi za serikali zinawezadhibiti tabia mbaya ya taasisi za fedha na mabenki kama picha hapo juu inavyoonesha. Ni bayana kuwa siku