Jinsi mawaziri wa fedha walivyodhibiti viwango vya riba na akiba



Kiwango cha riba na akiba za mabenki ni chombo muhimu sana kwa kukuza biashara na uchumi. Hii ni kwa sababu viwango viliopo huchangia kuvutia ama kutimua wateja ambao mara nyingi huwa ni wafanyibiashara. Kiwango cha kukopa kikiwa juu, wakopi hushindwa kulipa madeni yao. Lakini, wakopeshaji  wakiwa na mioyo ya kibepari kama Shailoki wa Venisi, hukimbilia  kuuza mali yao bila huruma wakidai walipwe kwa ‘haki na haka ya hati yao’.


Kenya, kama nchi, imelaumiwa  kwa kuwa na kiasi kidogo cha uwekezaji wa  akiba. Hata hivyo, wakosoaji  wamekataa kutambua kuwa faida ya mtu kuziacha pesa benki ni duni. Hii ni kufuatia  kuwa mvuvumko wa bei ya bidhaa mara nyingi huwa juu kushinda mapato yanaolipwa na hazina za benki  au taasisi zingine za kifedha. Hali hii huwatoa watu hamu ya kuwaacha pesa kwa akaunti  ya hazina.








Lakini juhudi za serikali zinawezadhibiti tabia mbaya ya taasisi za fedha na mabenki kama picha hapo juu inavyoonesha. Ni bayana kuwa siku za zamani kidogo, viwango za riba viikuwa vimedhibitiwa na hivyo vilikuwa na adabu. Nyakati za James Gichuru, Mwai Kibaki na Arthur Magugu kama mawaziri wa fedha (1963-1988) upenu kati ya kiwango cha kuwekeza na cha kukopa kilikuwa chini -yani si zaidi ya mara dufu. 


Ila , wazimu ulingia (1988-1992) wakati George Saitoti alikuwa kwenye usukani. Kwa bahati nzuri Musalia Mudavadi alipongia, alifanya juhudi kupindua mtindo na kiwango cha kukopesha kikaanza kushuka. Mtindo huo  uliendelea hadi David Mwiraria na Uhuru Kenyatta walipolegea kazini. Lakini, kwa bahati nzuri tena, Robinson Githae alikaidi mtindo huo mapema kwenye mwaka wa (2011) na mambo yameebakia  shwari hadi leo.


Hivyo basi, sheria ya kudhibiti viwango vya riba ni sharti iendelee kuungwa mkono hata kama wakopeshaji wamehodhi  pesa na kukataa kupeana mikopo wakidai eti watapata hasara. Nia na mbinu zao mbovu za biashara ziendelee kukashifiwa wa wote nchini.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FALSAFA

IKTISADI

Katiba kwenye mtazamo wa miraba tatu (Sehemu II-I): Kugeuza katiba bila Kura ya maoni