IKTISADI



Iktisadi ni nini?

Iktisadi ni sayansi ya kijamii inayo husika na jinsi matarajio na mahitaji mengi ya jamii yanawezatoshelezwa na raslimali haba.

Wanaiktisadi ni wanasayansi na kwa hivyo wanawezakutoa kauli mbili: kauli thabiti na kauli ya kimapendekezo.

Kauli thabiti: Hizi ni kauli zinazowezadhibitishwa kwa kufanyiwa utafiti, kwa mfano: bei zikishuka, bidhaa zitanunuliwa kwa wingi zaidi.

Kauli pendekezi: Haya ni mapendekezo tu, kwa mfano: Serikali inafaa ipunguze ushuru kwa bidhaa muhimu. Hivyo basi, wanaiktisadi mara nyingi hawaakifikiani.

KUUNDA MODELI/NATHARIA

1. Jumlisha dhana
2. Tunga miongozo
3. Dhibitisha miongozo
4. Matokeo yakitoshana na = ukweli wa mambo
5. Basi inakuwa natharia

Modeli husaidia kurahisisha kuelezea dhana tofauti tofauti. Katika somo la kiuchumi, modeli/natharia huchukua mfano ya chati.

Raslimali za kiuchumi:

Pia zinawezaitwa Viungo vya Kuzalisha Uchumi navyo ni

1. Ardhi – Raslimali yote halisi iliyopo pahali fulani.
2. Leba–Bidii ya kutumia misuli na akili 
3. Mtaji – Uwekezaji wa mali zote zisizo halisi.
4. Tarazaki –Bidii ya kujumlisha viungo hizo tatu ili kuzalisha bidhaa na huduma.


MATAWI YA IKTISADI

1. Iktisadi Finyu: Inashugulika na maswala ya kambuni ama sekta ya
2. Iktisadi Pana: Inashughulika na uchumi wa nchi, fedha na biashara ya kimataifa






MIFUMO ZA KIUCHUMI

Mfumo wa kiuchumi ni jinsi uchumi umeundwa na kuenezwa. (Pia jinsi maswali nyeti yanavyo jibiwa).

Hukuna hali kama mfumo pangwa kamilifu au huru kamilifu. Nchi zote zimechanganya hali hizi mbili kwa kiasi fulani.
  


Kuna, kwa msingi, aina tatu za mifumo za kiuchumi duniani nazo ni
1. Pangwa (Ujamaa)
2. Huru (Ubinafsi)
3. Mchanganyiko


Tofauti kati ya mahitaji na mapambo


MAHITAJI:
Hizi ni bidhaa muhimu katika maisha ya binadamu. Na zinajumlisha chakula, makao na mavazi.

MAPAMBO:
Hizi ni bidhaa ambazo zinaongeza starehe katika maisha ya wanadamu nazo zinajumlisha televisheni, rununu, gari n.k.

UHABA
Uhaba ndio shida kuu ya kiuchumi. Hakuna wakati ambapo mtu, jamii kambuni ama nchi itakuwa na raslimali nyingi hata ikakosa haja ya kuitunza.

Ni uhaba huu unaofanya jamii zote kuboresha njia za kufanya uamuzi baina ya mapendekezo yaliopo.


MASWALI MAALUM YANAYO WAKABILI WANAUCHUMI

1. Nini kizalishwe?
2. Kwa kiwango kipi?
3. Kizalishwe vipi?
4. Kizalishwe wakati gani?
5. Kuzalishia nani?
6. Kuzalishia wapi?

Kila chaguo ina hasara yake. Katika somo la iktisadi hasara inayoletwa kwa kutupilia mbali pendekezo ilikuchagua pendekezo ingine ni hasara ya hitari.


HASARA YA HITARI: Ni ile kupotea kwa faida ingalililetwa na pendekezo iliyotupiliwa mbali.

Hata hivyo wanauchumi huonelea kuwa watu hutumia busara kila wanapofanya maamuzi kwa hivyo pendekezo linalochaguliwa huwa ni lile lenye kuleta faida kubwa kushinda lile ambalo halikuchaguliwa.



Tofauti kati ya mfumo pangwa na mfumo huru
Mfumo huru

1. Raia wanamiliki viungo vya uzalishaji
2. Faida ndio dhamira ya uzalishaji
3. Mteja ndio mfalme
4. Soko linaamua bei
5. Kuna ushindani sokoni
6. kupunguza hasara ni muhimu

Mfumo pangwa

1. Serikali inamiliki viungu vya usalishaji
2. Kutosheleza umma ndio dhamira ya uzalishaji
3. Serikali ndio mfalme
4. Serekali inamua bei
5. Hakuna ushindani sokoni
6. Usawazishaji ni muhimu


Ubora wa mfumo huru
·         Bidhaa za hali ya juu
·         Uchumi unapanuka haraka
·         Maendeleo ni mengi
·         Raslimali inatumika kikamilifu
·         Aina nyingi za bidhaa sokoni
·         Watu wengi wanaridhishwa

Upungufu wa mfumo huru
·         Pengo kubwa baina matajiri na maskini
·         Bidhaa ni za hali ya chini
·         Bidhaa hatari zinawezauzwa
·         Mazingira yanaharibiwa
·         Ushindani unaweza kuwa mkali kupindukia
·         Bei ya bidhaa inapaa
·         Sehemu zingine zinastawi zaidi kuliko zingine
Ubora wa mfumo pangwa

·         Inapunguza pengo kati ya matajiri na fukara
·         Bidhaa duni hazizalishwi
·         Mazingira haiharibiwi
·         Ajira zinahifadhiwa
·         Bei zinadhibitiwa


Upungufu wa mfumo pangwa

·         Uchumi inalimatia
·         Maendeleo ni machache
·         Bidhaa ni za aina kidogo
·         Watu hawatoshelezwi kikamilifu
·         Ubunifu uko chini




MWAFAKA WA BEI

Katika soko huru mivuto ya hamu ya kununua na hamu ya kuuza ndio huamua bei ya bidhaa


HAMU (GHASHI) YA KUNUNUA: Ni hamu ya mnunuzi kutaka kununua bidhaa au huduma ikiwa imewekewa bei fulani.

HAMU (DHATI) YA KUNUNUA: Ni madhumuni ya mnunuzi kununua bidhaa au huduma kiasi fulani kwa bei maalum.


Mambo yanayodhuru (ghashi) hamu ya kununua

·         Ubora k.v. rangi, uzito, nguvu n.k
·         Hitari na kuthamini ya kibinafsi
·         Matangazo ya kibiashara
·         Uwepo wa bidhaa hiyo sokoni
·         Idadi ya watu
·         Sera za serekali
·         Mahali
·         Mapato ya mnunuzi



Mambo yanayodhuru (dhati) hamu ya kununua

Ni moja tu nayo ni BEI (yake) na bei ya bidhaa badala au bidhaa ambatani)

KAULI YA HAMU YA KUNUNUA

Mambo yote yakisalia sare, bei ya bidhaa ikipanda, hamu dhati ya kununua bidhaa hiyo itashuka. Yani kuna uhusiano kinzani baina ya bei na kiasi cha bidhaa.

HAMU (GHASHI) YA KUUZA: Ni hamu ya muuzaji kutaka kuuza bidhaa au huduma ikiwa imewekewa bei fulani.


HAMU (DHATI) YA KUUZA: Ni madhumuni ya muuzaji kutaka kuuza bidhaa au huduma kiasi fulani kwa bei maalum.


Mambo yanayodhuru hamu (ghashi) ya kuuza

·         Gharama ya uzalishaji
·         Sera za serekali (ushuru ama usaidizi)
·         Uwepo wa raslimali
·         Hali ya anga
·         Idadi ya wazalishaji
·         Teknolojia
·         Matarajio ya msalishaji
·         Wepesi wa kuifadhi bidhaa.


Mambo yanayodhuru hamu (dhati) ya kuuza

Ni moja tu nayo ni BEI ya bidhaa



KAULI YA HAMU YA KUUZA: Mambo yote yakisalia sare, bei ya bidhaa ikipanda, hamu dhati ya kuuza bidhaa hiyo itapanda. Yani kuna uhusiano sambamba baina ya bei na kiasi cha bidhaa.







Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FALSAFA

Katiba kwenye mtazamo wa miraba tatu (Sehemu II-I): Kugeuza katiba bila Kura ya maoni