FALSAFA
Falsafa
ni nini?
Falsafa
ni juhudi ya kuuliza, kufahamu na kujibu maswali sugu kwa tafakuri.
FALSAFA YA KIAFRIKA NA YA ULAYA
FALSAFA YA KIAFRIKA
Inaweza
kugawanywa katika sehemu zifuatazo mbili. Yani, falsafa ya Kiafrika ni aidha
Kiujumla:
Falsafa yoyote ile ambayo itaguzia maudhui ya kiafrika au itatumia mbinu za
kiafrika kukidhi madhumuni yake.
Kimaalum:
Falsafa ile tu imetokana na mtu ambaye ni Mwafrika au an uzao wa Kiafrika.
Falsafa
ya Kiafrika inachukua daraja tatu
1. Uhenga-tamaduni: Weledi wa mambo yote ya mila ya watu wa jamii fulani.
Hapa
kuna
Falsafa-tamaduni:
Weledi wa mila na desturi za jamii na unamilikiwa na watu wote wa jamii hiyo
ila, wazee ni wahenga zaidi kuliko watoto.
Falfasa-uhenga:
Weledi wa mambo ya mila na tamaduni za jamii zilizomo kwenye mhenga mmoja
mashauri.
Falsafa-shehe:
Mweledi wa mambo ya mila na tamaduni za jamii pamoja na mambo mengi ya
malimwengu
2.
Falsafa-itikadi: Uanzilishi ama uzinduzi wa mfumo wa fikira wa kufuatwa na
wananchi wote. Hii ilitokana na mataifa ya Afrika kujinasua kutoka kwa ukoloni.
Waanzilishi wa mataifa kama Mwalimu Nyerere, Kwame Nkuruma na Leopold senghor
walikuwa na maono thabiti ya kuelekeza mataifa yao.
3. Falsafa-taaluma: misimamo zinazotolewa na wafalsafa ambao wanayaandika kinagaubaga k.m. Ngugi wa Thiong’o (kukomboa ubongo)
Maono-mlimwengu
ya falsafa ya kiafrika huchukua mfumo:
MUNGU
(MIUNGU)—MAPEPO---BINADAMU—VITU HAI---VITU VISIYO NA UHAI
FALSAFA
YA ULAYA
Inaanzia
na ile ya Wayunani hadi wafalsafa wa siku hizi. Ina historia ndefu kushinda ile
ya kiafrika kwa sababu walianza kuandika mambo yao zamani na kuwaza kuziifadhi
hati hizo vyema.
MATAWI
YA FALFASA
Falsafa
inagawanyika kwa matawi tanu maalum
1. Asilia: Ni fani ambayo inatafuta asili ya vitu ama mambo zaidi kuliko na halisi yao.
Inajumlisha
vitu vyote ulimwenguni pamoja na malimwengu. Inauliza maswali kama:
Dunia /ulimwengu
upo kweli? Je Mungu yupo? Tukikufa mioyo zetu huenda wapi?
2. Ufahamu: Ni somo linalohusu ‘fahamu’.
Linazingatia maswali kama:
Naweza
kujua nini? Ufahamu unapatikana vipi? Ukweli unadhibitishwaje?
Matawi
ya Ufahamu
i)
Taamuli- kutambua mambo kwa kutumia akili
ii)
Hisia- kutambua mambo kwa kutumia viungo vya mwili yani macho, masikio, pua,
mikono na ulimi.
3. Thamani:
A. Sanaa:
Maswala kuhusu urembo, nakshi, (ma)umbo na urari.
B.
Maadili: Maswala kuhusu jinsi binadamu anastahili kutekeleza mambo. Ina sehemu
tanu zifuatazo
i) Asili
ya maadili: Maswali yake makuu ni- Je, maadili kweli yako? Yanatoka wapi? Nini kizingatiwe
wakati wa kuamua jambo ni nzuri au baya? Na je, kuna kitu kama tabia nzuri?
ii)Msingi
wa maadili: Maswali yake makuu ni- Tutafikiaje kiwango kizuri cha kutathmini
maadili kama vile amri kuu ‘tendea mwenzako jinsi ungependa wewe utendewe’
iii)Maadili
ya utendakazi: Maadili katika taaluma mbali mbali kwa mfano- Wanasheria,
Wanahabari, Madaktari n.k.
iv)Saikolojia
ya utu: Inashuhudia swala kama- Umri wa kuwajibika kwa watoto
v)Maadili
ya dharura: (Maadili huru) Inashuhudia jinsi watu wanavyokabiliana na juhudi
zao kila siku na hivyo jinsi maadili yao yanavyodhihirika yenyewe.
4. Dabiri: Jinsi ya kurazini vyema.
Inatumiwa na wanafalsafa kutafuta na kudhibitisha ukweli katika mambo yote.
Inajumlisha mambo kama nususi na ukimu. Taratibu zake mbili ni:
i) Kutohoa:
Inazingatia kutafuta ukweli mahususi kutoka na ukweli pana uliopo
k.m.
(kama) binadamu wote wana uhai
(na
pia) Kamau ni binadamu
(hatima
yake basi) Kamau ana uhai
ii) Kulimbikiza:
Inazingatia kutafuta ukweli pana kutoka kwa ukweli mahususi uliopo.
k.m.
(kama) Kamau ana uhai
(kama) Omondi ana uhai
(na
pia) Kamau na Omondi wote ni binadamu
(hatima
yake basi) Binadamu wote wana uhai
* Matawi
haya manne yanatengemeana kwa kufanikisha jukumu zao. Bila ufahamu hakuna jambo
linalowezaeleweka; na, kueleweka, lazima chanzo na kiini cha kitu hicho
kijulikane; kiini cha kitu hakiwezijulikana bila maswali sugu kuulizwa na
majibu ibuka kupigwa tarubini kwa dabiri; lakini, dabiri haiwezifanywa kwa
ukamilifu bila kuzingatia maadili; nayo, maadili lazima yadhibitishwe kwanza
yapo (kwa kutegemea falsafa asilia)na yana msingi(kwa kutegemea ufahamu).
5. Siasa: Jinsi ya kutawala vyema
NUSUSI KUHUSU FALSAFA
1. Falsafa sio somo maalum ila ni mbinu katika
masomo au fani zozote kwa ujumla. Pia inawezasemwa kuwa ni kitovu cha usomi
wote.
2.
Falsafa inalenga sana maswali kuliko majibu. Kwa hivyo hata jibu likitolewa falsafa
itauliza kama jibu hilo ni la kweli au la.
3.
Falsafa hubadilika baada ya muda fulani kulingana na mambo yanaowakabili watu
katika enzi yao na pia mahali ambapo inafanywa kwa mfano: sokoni, makanisani,
vyuoni, kwenye migongamano na, katika mtandao
UMHIMU WA KUSOMA FALSAFA
1.
Falsafa inatusukuma kuwaza kwa undani kuhusu mambo yote hata yale
tunayoyachukulia kuwa kawaida.
2. Ina
faida katika taaluma nyingi kama vile uanasheria, usamamizi, uanahabari,
utafiti na udaktari ambapo kufikiri kwa undani zaidi na kupata majawabu yasiyo
bayana kwa watu wote.
3. Ina
faida katika kazi nyingi kwa sababu hutoa mwelekezo thabiti kwa mambo ya
maadili
4.
Falsafa ni somo pana kwa hivyo humpa mtu (mwanafunzi au mtaalam) ujuzi na
fikira pana na kuwafanya kuwa watetezi na wahudumu wema zaidi
5. Pia
huwapatia watu mbinu za kufanya utafiti bora na tena kunoga ujuzi wa kujadili,
kuchambua, kuzingatia misimamo tofauti na kurasimu mawasiliano yao
6.
Falsafa inakusaidia kuwa binadamu bora ambaye anachangia kikamilifu kwa uwezo
wake wote wa kielimu.
*
Falsafa si fani/ kazi ya watu wa kale tu, au wanachuoni na wataalam maalum ila
inafaa kuwa juhudi ya watu wote katika harakati ya kuboresha maisha ya wote.
Maswali kama, ni nini kizuri, nini kibaya, nini kinastahili, na nini
hakistahili hayawezi kuwachiwa watu wachache tu.
Kazi nzuri
JibuFuta