Falsafa ni nini? Falsafa ni juhudi ya kuuliza, kufahamu na kujibu maswali sugu kwa tafakuri. FALSAFA YA KIAFRIKA NA YA ULAYA FALSAFA YA KIAFRIKA Inaweza kugawanywa katika sehemu zifuatazo mbili. Yani, falsafa ya Kiafrika ni aidha Kiujumla: Falsafa yoyote ile ambayo itaguzia maudhui ya kiafrika au itatumia mbinu za kiafrika kukidhi madhumuni yake. Kimaalum: Falsafa ile tu imetokana na mtu ambaye ni Mwafrika au an uzao wa Kiafrika. Falsafa ya Kiafrika inachukua daraja tatu 1. Uhenga-tamaduni: Weledi wa mambo yote ya mila ya watu wa jamii fulani. Hapa kuna Falsafa-tamaduni: Weledi wa mila na desturi za jamii na unamilikiwa na watu wote wa jamii hiyo ila, wazee ni wahenga zaidi kuliko watoto. Falfasa-uhenga: Weledi wa mambo ya mila na tamaduni za jamii zilizomo kwenye mhenga mmoja mashauri. Falsafa-shehe: Mweledi wa mambo ya mila na tamaduni za jamii pamoja na mambo mengi ya malimwengu 2. Falsafa-itikadi: Uanzilishi ama uzinduzi wa mfumo wa fikira wa ku
Iktisadi ni nini? Iktisadi ni sayansi ya kijamii inayo husika na jinsi matarajio na mahitaji mengi ya jamii yanawezatoshelezwa na raslimali haba. Wanaiktisadi ni wanasayansi na kwa hivyo wanawezakutoa kauli mbili: kauli thabiti na kauli ya kimapendekezo. Kauli thabiti: Hizi ni kauli zinazowezadhibitishwa kwa kufanyiwa utafiti, kwa mfano: bei zikishuka, bidhaa zitanunuliwa kwa wingi zaidi. Kauli pendekezi: Haya ni mapendekezo tu, kwa mfano: Serikali inafaa ipunguze ushuru kwa bidhaa muhimu. Hivyo basi, wanaiktisadi mara nyingi hawaakifikiani. KUUNDA MODELI/NATHARIA 1. Jumlisha dhana 2. Tunga miongozo 3. Dhibitisha miongozo 4. Matokeo yakitoshana na = ukweli wa mambo 5. Basi inakuwa natharia Modeli husaidia kurahisisha kuelezea dhana tofauti tofauti. Katika somo la kiuchumi, modeli/natharia huchukua mfano ya chati. Raslimali za kiuchumi: Pia zinawezaitwa Viungo vya Kuzalisha Uchumi navyo ni 1. Ardhi – Raslimali yote halisi iliyopo paha
Istilahi ‘Kura ya Maamuzi’ sasa imeanza kutumika ni kama ni sawia na kugeuza katiba. Katika mijadala nyingi zinazohuzisha akina yakhe, na nyakati zingine hata wataalam; kuna mwegemeo unaolenga kuashiria kuwa hakuna jinsi ingine ya kurekebisha katiba (kwa juhudi pana) bila kupiga kura hiyo. Imesemwa na kubalika kuwa asilimia 20 ya katiba ina kasoro, ila hakujakuwa na makubaliano ya ni nini ndio kasoro mahususi inayozungumziwa. Kila mtathmini ana maoni yake tofauti. Hiyo basi, huenda kupata uwiano dhabiti kwenye swala hili utachukua muda mrefu sana. Hati hii ya katiba ilikosa kizungu cha kutosha. Imebahatisha matumizi ya istilahi Marekebisho kumaanisha geuzo lolote katika katiba. Ilhali, katiba ya Marekani hutumia neno hilo kumaanisha kuboresha au kuimarisha hoja ama sheria, hapa Kenya tumewai kulitumia kumaanisha geuzo lolote bila kujali athari epuka. Hivo basi, katiba ya 1963 ilifanyiwa Marekebisho mengi ingawa yakiwa ya ubomofu na kudunisha sheria. Basi, itafaa Su
Maoni
Chapisha Maoni