Katiba kwenye mtazamo wa miraba tatu (Sehemu II-I): Kugeuza katiba bila Kura ya maoni
Istilahi ‘Kura ya Maamuzi’ sasa imeanza kutumika ni kama ni sawia
na kugeuza katiba. Katika mijadala nyingi zinazohuzisha akina yakhe, na nyakati
zingine hata wataalam; kuna mwegemeo unaolenga kuashiria kuwa hakuna jinsi
ingine ya kurekebisha katiba (kwa juhudi pana) bila kupiga kura hiyo.
Imesemwa na kubalika kuwa asilimia 20 ya katiba ina kasoro,
ila hakujakuwa na makubaliano ya ni nini ndio kasoro mahususi inayozungumziwa.
Kila mtathmini ana maoni yake tofauti. Hiyo basi, huenda kupata uwiano dhabiti
kwenye swala hili utachukua muda mrefu sana.
Hati hii ya katiba ilikosa kizungu cha kutosha. Imebahatisha matumizi ya istilahi Marekebisho kumaanisha geuzo lolote
katika katiba. Ilhali, katiba ya Marekani hutumia neno hilo kumaanisha kuboresha
au kuimarisha hoja ama sheria, hapa Kenya tumewai kulitumia kumaanisha geuzo
lolote bila kujali athari epuka. Hivo basi, katiba ya 1963 ilifanyiwa Marekebisho mengi ingawa yakiwa ya
ubomofu na kudunisha sheria. Basi, itafaa Sura ya 16 yenye kichwa: MAREKEBISHO
YA KATIBA HII itoe ufafanuzi wa
neno hilo Marekebisho ili tusirejelee makosa ya hapo nyuma.
Isitoshe, waadishi aidha walipungukiwa kwa utaalam wa
uandishi wa hati za aina hii, au walikosa ujuzi wa mawasiliano ya kiufundi. Hati
hiyo imewasilshwa kwa mfumo wa ripoti na pendekezo zaidi kuliko mfumo wa
mwelekezo. Upungufu huu unadhihirika tena kwenye sharia ya Kambuni na pia zenye
kuunda mashirika mengi ya umma.
Kuzuia uwezekano wa kurudishwa nyuma katika hatua zilizopigwa,
inawezakuwa heri kutofautisha ngazi za ubadilishaji wa hati kwa kuleta msamiati
mpya kama ifuavyo,
Kubadilisha: Utunzi
wa hati mpya ambayo ina mkusanyiko wa uhariri, usahihishi, urekebishi, na/ ama ustawishi
yenye nia ya kupindua kabisa hati hiyo.
Kustawisha: Hiyo pachiko
ambayo inastawisha ama kuboresha manuio yaliyomo kwenye Hati ya Haki; ama
kupendekeza haki ingine mpya.
Kurekebisha: Ile
kuongeza, kuhamisha, au kutoa afisi ya uakilishaji / jukumu; au hadhi ya afisi
/ maafisa.
Kusahihisha: Ile
kuongeza, kuhamisha, au kutoa afisi huru / / jukumu; au hadhi ya afisi / maafisa
Kuhariri: Kugeuza
maneno, vishanzi, vifungu, sehemu ya hati iliyopo iliongeza usanifu na/ama
ufasaha. Ila, uhariri hautakiwi kugeuza maana ya awali.
Kugeuza: Yote
hapo juu
Kifungu 255 (1) (a) – (j) [ya sura 16] kimearidhisha ‘hoja 10
nyeti ‘ ambazo lazima kura ya maoni iamue kugeuzwa kwao. Ilihali, hoja hizo 10
zilitundikwa pamoja mbelini labda kwa ukosefu wa muda, ni vyema sasa, kurejelea na
kukagua na kupanga hoja hizo kwa makundi maalum kama ifuatavyo,
Swala
|
Mchakato
|
Toleo
|
Jinsi geuko linavyodhihirika
|
Mkusanyiko wa haririsho, sahihisho,
rekebisho, na/au stawisho ambayo ina nuia kupindua kabisa hati iliyopo.
|
Kubadilisha
|
Badilisho
|
Nje ya hati; na kupindua hati ya awali.
Hati mpya inachukua mwaka wa uzinduzi k.m. Katiba 1963, 2010 n.k.
|
Hati ya Haki
c) mamlaka ya watu
e) Hati ya Haki
(a) mamlaka ya Katiba
(b) mipaka ya Kenya
|
Kustawisha
|
Stawisho
|
Kama pachiko na kujumlishwa
kwa tarakimu k.m. 1, 2, 3 n.k.
|
Uakilishi
(f) kipindi cha urais
h) majukumu ya Bunge
(i) malengo, kanuni na muundo wa serikali ya ugatuzi
|
Kurekebisha
|
Rekebisho
|
Ndani ya hati; na kupindua
Sehemu, *kishanzi, kipengee, au sura ya awali.
|
Afisi huru; Maadili ya kitaifa, Kanuni za kiutawala
(g) uhuru wa Idara ya
Mahakama, Tume, na afisi huru zinazorejelewa katika Sura ya Kumi na tano
(d) maadili ya kitaifa, kanuni za kiutawala zilizoorodheshwa katika
Kifungu cha 10(2) (a) hadi (d)
|
Kusahihisha
|
Sahihisho
|
Ndani ya hati; na kupindua
Sehemu, *kishanzi, au sura ya awali.
|
Kurejelea/ Rudufu/ Pangilia
(j) mwelekezo wa Sura 16
|
Kuhariri
|
Haririsho
|
Ndani ya hati; na kupindua maandishi (neno, *kishanzi, kifungu,
sentensi) ama akifisho ya awali.
|
Baadhi/au yote hapo juu
|
Kugeuza
|
Geuzo
|
Kama ilivyo *thaminiwa kwa kila kumbo
|
Tunavyo endelea kukuwa kidemokrasia na mifumo ya uongozi, ni sharti tuendelee kubuni mbinu na kuongeza
maarifaa ili tuweze kulinda maendeleo ipasavyo.
Ikiwa ni kweli kuwa asilia 80 ya katiba ni nzuri, basi lazima megeuzo
yoyote mapya yasidhulumu wema huo.
Isipokuwa ‘hoja 10 nyeti ‘ katika Kifungu 255 (1) (a) – (j),
katiba inaweza kugeuzwa bila kura ya maamuzi kama ilivyosawiriwa hapa juu.
Edwin Musonye & Patrick
Musindi
Mawasiliano ya Kiufundi, kambuni
ya Document Point
Maoni
Chapisha Maoni